Powered By Blogger

Friday, August 19, 2016

PIGO JINGINE KWA LVERPOOL HII LEO

SADIO MANE AUMIA   KUIKOSA BURNLEY.


MSHAMBULIAJI wa Liverpool, Sadio Mane anaweza kushindwa kucheza mchezo wa kesho dhidi ya Burnley.

Mchezaji huyo ambaye alionyesha kiwango kizuri kwenye mchezo dhidi ya Arsenal, wikiendi iliyopita, anatarajiwa kukosa mchezo huo baada ya vipimo kuonyesha kuwa ana matatizo ya misuli ya bega.

Mane alipelekwa hospitalini kutazamwa bega baada ya kuumia kwenye mazoezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Melwood.

Hata hivyo, vipimo vimeonyesha kuwa mchezaji huyo ameumia mfupa wa bega lakini halijachomoka hali ambayo ilimpa ahueni Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp.

Taarifa zinasema ataendelea kuangaliwa na madaktari wa timu hiyo na ana asilimia ndogo ya kucheza mechi dhidi ya Burnley.

Mane ambaye alifunga bao moja Jumapili iliyopita kwenye ushindi wa timu yake dhidi ya Arsenal alijiunga na Liverpool akitokea Southampton kwa pauni milioni 30.

No comments:

Post a Comment