Powered By Blogger

Sunday, August 21, 2016

OFFICIAL- JOEL CAMPBELL ATIMKIA NCHINI URENO



Sporting Lisbon ya Ureno imetangaza kumsajili kwa mkopo wa msmu mzima mshambuliaji wa Arsenal na Costa Rica Joel Campbell.
Campbell, ambaye ameifungia Arsenal magoli manne kwenye michezo 30 katika michuano yote kwenye msimu wa 2015-16, amejiunga na timu hiyo kwa mantiki ya kupata nafasi ya kucheza zaiidi katika kikosi cha kwanza.
Campbell ,24, alijiunga na Arsenal mwaka 2011 akitokea timu ya Deportivo Saprissa ya nchini Costa Rica na ameshatolewa kwa mkopo mara tano tangu ajiunge na Washika bunduki hao.
Msimu wa 2012-13, Campbell alipelekwa kwa mkopo kwenye klabu ya Ligue 1 ya Lorient, akafunga magoli manne kwenye michezo 27, kabla ya kupelekwa klabu ya Real Betis kwenye msimu uliopita..
2013-14 alienda Olympiacos, na kufunga mabao 11 ikiwemo kwenye mechi ya klabu bingwa dhidi ya Manchester United kwenye hatua ya 16 bora..
Alipelekwa tena kwa mkopo kwenda Villarreal msimu wa 2014-15, kabla ya kurudi tena Arsenal msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment