BRAZIL WANYAKUA MEDALI YA DHAHABU OLIMPIKI SOKA, WAINYOA UJERUMANI KWA MATUTA
Wachezaji wa Brazil wakiongozwa na Nahodha wao, Neymar (katikati) wakishangilia baada ya kushinda Medali za Dhahabu za Michezo ya Oilimpiki 2016 Uwanja wa Maracana mjini Rio usiku wa jana kufuatia ushindi wa penalti 5-4 baada ya sare ya 1-1. Brazil ilitangulia kwa bao na Neymar dakika ya 27, kabla ya Max Meyer kuisawazishia Ujerumani dakika ya 59. Neymar akaenda kupiga na kufunga penalti ya ushindi, baada ya mkwaju wa Nils Petersen kuokolewa
No comments:
Post a Comment